Ngozi Okonjo-Iweala aonya kuhusu ubaguzi katika usambazaji wa chanjo
Ngozi Okonjo-Iweala, Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Biashara Ulimwenguni (WTO), ameonya dhidi ya "ubaguzi"

Ngozi Okonjo-Iweala, Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Biashara Ulimwenguni (WTO), ameonya dhidi ya "ubaguzi" katika usambazaji wa chanjo dhidi ya corona.
Okonjo-Iweala ambaye hapo awali alikuwa Kiongozi wa Chama cha Chanjo Duniani (GAVI)
ameiambia BBC,
"Wakati nchi tajiri zikiwapatia chanjo raia wao, nchi masikini hazipaswi kusubiri chanjo."
Okonjo-Iweala amesema kuwa katika wiki za hivi karibuni, nchi nyingi zimekuwa zikijaribu kuzuia usafirishaji wa chanjo zinazotengenezwa ndani ya mipaka yao, na kubainisha kuwa hali hii itazuia ahueni ya ulimwengu.
"Hakuna nchi inayoweza kujisikia salama ikiwa kila nchi itafikiria watu wake.", alisema.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Antonio Guterres pia amezitaka nchi zote kuwa na 'mshikamano' na kuondoa 'utaifa wa chanjo' kwa kuunga mkono chanjo kwa watu wote.
Habari Zinazohusiana
Diaz-Canel achukuwa nafasi ya Castro Cuba
Rais wa Cuba Miguel Diaz-Canel ateuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Kikomunisti cha Cuba

Kiapo cha uaminifu kwa serikali Hong Kong
Maafisa wa umma wasiokula kiapo cha uaminifu kwa serikali Hong Kong kufutwa kazi