Mapigano ya kikabila Sudan
Watu kumi wamepoteza maisha katika mapigano kati ya makabila mawili
1594881
Watu kumi wamepoteza maisha katika mapigano kati ya makabila mawili katika jimbo la Darfur Kaskazini la Sudan.
Kulingana na shirika rasmi la habari la Sudan SUNA, mzozo kati ya makabila ya Fur na Tama wenye asili ya Kiafrika katika eneo la Seraf Omra Kaskazini mwa Darfur umegeuka kuwa mzozo juu ya ardhi na uongozi.
Watu 10 wamefariki katika vita, watu 32 wamejeruhiwa.
Matukio hayo yalidhibitiwa katika mkoa huo, ambapo serikali iliweka amri kamili ya kutotoka nje.
Wakati majeruhi walipelekwa hospitalini, washukiwa wengine wa tukio hilo waliwekwa chini ya ulinzi.
Habari Zinazohusiana

Shambulizi la bomu Somalia: 5 wafariki
Wanajeshi 5 wafariki kwenye shambulizi la bomu lililolenga vikosi vya usalama nchini Somalia