Barcelona yatinga fainali Copa del Rey
Barcelona yaishinda Sevilla 3-0 kwenye mechi marudiano ya nusu fainali ya Copa del Rey

Barcelona ilikuwa timu ya kwanza kuingia fainali ya kombe la Copa del Rey nchini Uhispania baada ya kuishinda Sevilla 3-0 katika mechi ya marudiano ya nusu fainali.
Timu hiyo ya Catalonia ambayo ilishindwa 2-0 na Sevilla ugenini kwenye mechi ya kwanza ya nusu fainali, ilipindua matokeo hayo katika mechi ya marudiano kwa kufunga mabao 3.
Kipindi cha kwanza cha mechi kilimalizika wakati Barcelona inaongoza 1-0 kupitia bao lililofungwa na Ousmane Dembele dakika ya 12.
Baada ya muda wa kawaida wa mechi, Brcelona ilipata bao katika dakika za mwisho za ziada (Dak. 90 + 4) kupitia Gerard Pique na mechi ikaisha 2-0 na kulazimika kuchezwa muda wa nyongeza.
Mwanzoni mwa muda wa nyongeza, Martin Braithwaite alifunga bao katika dakika 95 baada ya kupokea pasi kutoka kwa Jordi Alba na kumalizika 3-0.
Barcelona ambayo imeshinda Kombe la Copa del Rey mara 30 na kuwa timu iliyocheza fainali nyingi zaidi (mara 41), na imeweza kucheza katika fainali mara ya 9 katika misimu 10 ya mwisho.
Katika nusu fainali nyingine ya Kombe hilo, Levante na Athletic Bilbao zitacheza usiku wa leo saa 23:00. Mechi ya kwanza iliyochezwa kwenye uwanja wa Bilbao ilimalizika 1-1.
Habari Zinazohusiana

Real Madrid yailaza Barcelona kwenye El-Clasico
Real Madrid yaondoka na alama 3 baada ya kuishinda Barcelona 2-1 kwenye dimba la El Clasico

Wanariadha wa Uturuki
Je unajua kwamba Uturuki ilipata medali nyingi katika Balkan kwenye mashindano ya mwaka 2020?