Lakers yaishinda Warriors 117-91 kwenye NBA
Mabingwa watetezi Los Angeles Lakers wapata ushindi dhidi ya Golden State Warriors kwenye NBA

Timu ya Los Angeles Lakers ambayo ndio bingwa wa mwisho wa Ligi ya mpira wa kikapu ya NBA nchini Marekani, ilipambana na Golden State Warriors usiku wa jana.
Ligi ya NBA iliendelea na mechi 7 zilizochezwa hapo jana.
Los Angeles Lakers ilifanikiwa kuondoka na ushindi muhimu baada ya kuipiga Golden State Warriors 117-91 kwenye mechi hiyo.
Baada ya kupoteza michezo nne mfululizo, Lakers ilianza kwa kasi kubwa mechi hiyo na kuongoza 41-21. Mabingwa watetezi wa Los Angeles walionyesha umahiri wao katika uwanja wao wa Staples Center na kumaliza kwa ushindi 117-91 dhidi ya Golden State Warriors.
Matokeo kamili ya mechi zote zilizochezwa usiku wa jana ni kama ifuatavyo:
Boston Celtics-Washington Wizards: 111-110
Houston Rockets-Memphis Grizzlies: 84-133
Miami Heat-Atlanta Hawks: 109-99
Detroit Pistons-New York Knicks: 90-109
Los Angeles Lakers-Golden State Warriors: 117-91
Minnesota Timberwolves-Phoenix Suns: 99-118
Sacramento Kings-Charlotte Hornets: 126-127
Habari Zinazohusiana
Olimpiki ya Tokyo kufanyika kama ilivyopangwa
Kamati ya maandalizi ya Michezo ya Olimpiki ya Tokyo yatangaza kuwa mashindano yatafanyika mwaka huu

Mechi za robo fainali zakakamilika UEFA Europa League
Manchester United, Roma, Arsenal na Villareal watinga nusu fainali UEFA Europa League